[SEHEMU YA 1]
Walakini, nilipokuwa chuoni, nilianza kuwa na mashaka kama malezi yangu au imani yangu ya kidini ilikuwa kweli au kama ilikuwa desturi na tamaduni tu.
Hivyo nilipokuwa natafuta majibu, nikaalikwa kujifunza Biblia na waumini wa Kanisa la Mungu.
Na wakati wa masomo ya Biblia, nilishangazwa sana na kile walichonionyesha katika Biblia.
Hivyo niliweza kuona kweli kwamba yale ambayo Kanisa la Mungu lilikuwa linafundisha yalikuwa halali, na bila shaka huu ni ukweli.
[SEHEMU YA 2]
Kati ya mambo yote niliyojifunza katika Kanisa la Mungu, naweza kusema jambo la kufumbua macho zaidi na kugusa zaidi kwangu lilikuwa kujifunza kuhusu Mungu Mama.
Na hilo lilikuwa jambo la kufumbua macho kwa sababu sikuzote tunaenda kanisani na kumwamini Mungu Baba, lakini hapa ni Biblia inayoshuhudia kuhusu Mama yetu wa Mbinguni, Mungu Mama.
Na nilipojifunza kwamba Yerusalemu Mpya, Bibi-arusi, mke wa mwana-kondoo alikuwa Mama yetu wa Mbinguni, nilishangaa pia kujifunza kwamba Alishuhudiwa tangu mwanzo wa Kitabu cha Mwanzo, Mungu Aliposema, “Tufanye mtu kwa mfano wetu na sura yetu.”
Hivyo imeonyeshwa dhahiri.
Imeonyeshwa dhahiri Mungu Mama Aliyeshuhudiwa kuanzia kitabu cha kwanza cha Mwanzo hadi kitabu cha mwisho cha Ufunuo.
Na nikaja kuelewa kwamba ushuhuda wa Mungu Mama upo tangu mwanzo wa Biblia.
Umejaa katika maandiko yote.
[SEHEMU YA 3]
Kumwamini Mungu Mama kwangu kulikuwa rahisi nilipojifunza Biblia, walakini, ilikuwa vigumu kidogo kuamini kwamba Mungu Mama Alikuja katika mwili.
Na ninafikiri jinsi ambavyo hatimaye niliweza kuelewa hilo ilikuwa kwa kuangalia nyuma kwa yale yaliyotukia kwa Yesu miaka elfu mbili iliyopita.
Na kupitia hilo, niliweza kutambua kwamba ili nimkubali Mama wa Mbinguni Aliyekuja katika mwili, sipaswi kumkaribia au kumwamini Mungu Mama kupitia mawazo, mitazamo, au dhana zangu zenye mipaka.
Na ninahitaji kumwona na kumwamini Mama wa Mbinguni kupitia unabii wa Biblia tu.
[SEHEMU YA 4]
Ikiwa kuna mtu yeyote mwenye wakati mgumu kumpokea Mungu Mama, ningemwambia aanze kumwelewa Mungu Mama kwa kuangalia uumbaji unaomzunguka.
Uhai hutoka kwa mama, hiyo ni sheria ya asili ya Mungu isiyobadilika ambayo Yeye Mwenyewe Alibuni.
Na sababu ya hilo ni kwamba Mungu Alitaka kutuonyesha kwamba hakuna Baba tu bali kuna Mama ambaye Anatupa uzima wa milele.
[SEHEMU YA 5]
Kabla sijaja katika Kanisa la Mungu, sikuzote nilikuwa na wasiwasi kuhusu kama nitafanya maamuzi sahihi maishani, na kama nitaweza kuishi maisha yangu ya pekee vizuri au la.
Walakini, baada ya kupokea ukweli na kujifunza kuhusu amri za Mungu, hatimaye nilhisi uhakika na nilikuwa na furaha na amani kwamba nitaweza kumtii Mungu na kuishi maisha yanayostahili kama mtoto wa Mungu na kuingia Mbinguni.
Ikiwa kuna mtu yeyote anayetafakari kuhusu kuja katika Kanisa la Mungu, ningependekeza njoo tu kila unapopata nafasi ya kujifunza Biblia.
119 Bundang S.L.P, Bundang-gu, Seongnam-si, Gyeonggi-do, Jam. ya KOREA
Simu 031-738-5999 Faksi 031738-5998
Makao Makuu: 50, Sunae-ro, Bundang-gu, Seongnam-si, Gyeonggi-do, Jamhuri ya Korea
Kanisa Kuu: 35, Sunae-ro, Bundang-gu, Seongnam-si, Gyeonggi-do, Jamhuri ya Korea
Jamii ya Misheni ya Dunia ya Kanisa la Mungu. Haki zote zimehifadhiwa. Sera ya Faragha